Kuna njia mbili za kufanya hivyo kwa kutumia DistroKid.
Njia moja ni kupakia albamu kamili iliyo na singo zote na kuweka tarehe ya mbeleni iliyopangwa kwa albamu kamili kutolewa. Hii itazalisha ISRC kwa nyimbo zote kwenye albamu. Baada ya albamu kupakiwa, unaweza kupakia kila singo kivyake na kwa tarehe yake ya kutoa, huku ukiingiza ISRC zake ambazo zilitolewa ulipopakia albamu. Unaweza kuingiza ISRC hizi kwenye fomu ya kupakia kwa kutumia chaguo la "tayari una msimbo wa ISRC?".
Njia nyingine ni kupakia kwanza singo zako kwa DistroKid kila moja kivyake, na kisha kutumia ISRC zinazozalishwa kwa singo hizi katika upakiaji wa albamu kamili hapo baadaye.
Katika hali yoyote, uko huru kufuta singo hizo kutoka kwenye maduka mara tu albamu inapotolewa, au kuziacha hewani pamoja na albamu!
Sign Up